RahmaMachuppa akifanya makamuzi yake jukwaani..
Muimbaji taarab wa chama kubwa Bongo Jahazi Modern Taarab bibie Rahma Machuppa hivi karibuni alikiri kwenda kwa waganga.
Muimbaji
huyo ambae anatamba na kibao chake cha 'Nipe Stara' kilichopo kwenye
albam mpya ya Jahazi aliongea huku akiwa na komfidensi zote alikiri
kwenda kwa waganga mara kwa mara kwa ajili ya kuweka nyota yake sawa na
kujitoa nuksi na mikosi lakini sio kwa lengo la kumroga mtu.
Mwanadada
huyo mwenye makeke na makomfinfidence ya ajabu awapo jukwaani alizidi
kufunguka katika kituo kimoja cha televisheni na kusema hata akiambiwa
na mganga akavunje 'nazi' mchana kweupe mbele ya adhala ya watu atafanya
ilimradi mambo yake yamnyookee. Pia alitoa ONYO KALI kwa yoyote
ataeenda kumroga kwani lolote litalompata asije akaenda kumuomba msamaha
maana hatokuwa tayari KUMSAMEHE KABISAA!!!
Haya wadada wa kibongo mnaoendaga kuroga alafu mnakataa kabisa kuwa amuamini mambo ya ushirikina MPOO!! Maana wengine mmejaa chale
mwili mzima alafu bado mwajifanya amuamini uchawi tuwaeleweje?? Wengine
tunawajua mnakeshaga kwa waganga HADI MKAKOSWAKOSWA KUOLEWA NA WAGANGA
alafu mnatudanganya amuamini ushirikina ndio nini!! Ebu kuweni na moyo
wa ujasiri kama Rahma jamani na sio kujifichaficha wakati ndio vinara wa
kukesha makaburini kuroga.
MNAJIJUWA!!
Mi nimemaliza kama una la zaidi toa comment apo tujue..
sOURCE: ZEddylicious
No comments:
Post a Comment