Mabingwa wa kombe la Vilabu
Bingwa Afrika Mashariki na Kati almaarufu kombe la Kagame, timu ya Young
Africans Sports Club imeifunga timu ya Black Leopard ya Afrika Kusini
mabao 3-2 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika leo jioni katika Uwanja
wa Taifa jijini Dar es salaaam.
Young Africans iliyokuwa nje ya
nchi kwa kambi ya mafunzo takribani wiki ilikuwa ikicheza mbele ya
washabiki wake, iliweza kucheza soka safi na la kuvutia kipindi chote
cha mchezo huku Black Leopard ikipata wakati mgumu kwa dakika 45 za
kipindi cha kwanza.
Didider Kavumbagu alikosa bao
la wazi dakika ya 21 ya mchezo akiwa yeye na mlinda mlango wa Black
Leopard Ayanda Mtshali, lakini shuti alilopiga lilipaa juu ya lango la
timu hiyo.
Yanga iliednelea kuutawala
mchezo kwa wachezaji wake kupigiana migongeo mizuri na kuutawala mchezo
hasa eneo la kiungo, Kabange Twite alishindwa pi akuipatia Yanga bao
katika dakika ya 25 baada ya kushinda kumalizia pasi safi ya Mbuyu
Twite.
Dakika ya 32 Jerson Tegete
aliipatia Young Africans bao la kwanza kwa mkwaju wa penati kufuatia
mlinzi wa Balck Leopard Harry Nyirenda kumuangusha Haruna Niyonzima
katika eneo la hatari, amabpo mwamuzi Hashim aliamuru upigwe mkwaju wa
penati na Jerson Tegete kuukwamisha mpira huo wavuni.
Yanga iliongeza kasi ya kusaka
bao la pili lakini shambulizi liliofanywa na Mbuyu Twite liliokolewa na
mlinda mlango wa Black Leopard Matshal kabla ya Mbuyu tena kupiga kichwa
kilichopaa mita chahce juu ya lango la timu ya Black Leopard.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika Young Africans 1 – 0 Black Leopard.
Kipindi cha pili kilianza kwa
Young Africans kufanya mabadiliko ambapo kocha Brandts aliwatoa Kabange
Twite, Mbuyu Twite na golikipa Ally Mustafa ‘Barthez’ nafasi zao
zikachukuliwa na Juma Abdul, Saimon Msuva na golikipa Said Mohamed.
Dakika ya 47, Humphrey Khoza
aliipatia Black Leopard bao la kusawazisha kwa kichwa akiunganisha mpira
wa kona uliopigwa na Edagr Manaka kufutia kutokuwepo kwa mawasilaino
kati ya mlinzi Nadir Haroub na mkinda mlango wake Said Mohamed.
Kiungo chipukizi Frank Domayo
aliipatia Young Africans bao la pili dakika ya 63 ya mchezo, akimaliza
pasi safi iliyopigwa na kiungo Haruna Niyonzima na mpira huo kumkuta
Domayo ambaye alimchambua mlinda mlango wa Black Leopard Mtishal na
kuhesabu bao la pili.
Dakika 10 baadaye mshambuliaji
Jerson Tegete aliipatia Young Africans bao la tatu kwa umakini
akimalizia pasi ya kungo mshambuliaji Saimon Msuva aliyewatoka walinzi
wa timu ya Black Leopard na kumpasia mfungaji aliyeukwamisha mpira huo
wavuni.
Jerson Tegete nusra angeipatia
Young Africans bao la nne, kufuatia lakini krosi iliyopigwa na Saimon
Msuva kuokolewa na mlinzi wa Black Leopard sentimeta chache pemebeni mwa
lango huku Tegete tayari akiwa tayari kwa kuukwamisha mpira huo.
Dakika ya 89, Black Leopard
ilijipatia bao la pili kwa mkwaju wa penati kupitia kwa mshambuliaji
wake Rodney Magalela kufuatia mlinzi wa kulia wa Young Africans kumcheza
madhambi mshambuliaji huyo katika eneo la hatari.
Mpaka mpira unamalizika Young Africans 3- 2 Black Leopard.
Kocha mkuu wa Yanga Ernest
Brndts amesema anashukuru timu yake kwa kupata ushindi huo wa leo, kwani
timu ya Black Leopard ni timu nzuri, imecheza vizuri lakini mwisho wa
siku vijana wangu walikuwa ni bora zaidi ndio maana wameibuk ana ushindi
huo.
Kambi yetu ya mafunzo nchini
Uturuki imetusaidia sana, wachezaji wanacheza kwa kujiamini wametulia
hawana presha ya mchezo, hali inayopelekea kucheza migongeano kwa
uhakika na hii ni dalili tosha kuwa tupo tayari kwa mzunguko wa pili wa
ligi kuu ya Vodacom alisema ‘Brandts’
Young Africans: 1.Ally Mustapha
‘Barthez’/Said Mohamed, 2.Mbuyu Twite/Juma Abdul, 3.Oscar Joshua,
4.Nadir Haroub’Cannavaro’, 5.Kelvin Yondani, 6.Athuman Idd ‘Chuji’,
7.Kabange Twite/Saimon Msuva, 8.Frank Domayo, 9.Didier Kavumbagu/Said
Bahanuzi, 10.Jerson Tegete/George, 11.Haruna Niyonzima
Black Leopard: 1.Ayanda
Mtshali, 2.Ernort Dzaga, 3.Nkosiyabo Xakane, 4.Harry Nyirenda,
5.Humphrey Khosa, 6.Munganga Djunga Jean, 7.Mongezi Bobe, 8.Thomas
Madimba, 9.Abbas Amidm, 10.Edagr Manaka 11.Rodney Ramagalela
No comments:
Post a Comment