SIKU chache baada ya kuwepo kwa madai kuwa modo ambaye pia ni Miss
Tanzania namba 2, 2006, Jokate Mwegelo amechumbiwa, mwanamuziki mkongwe
John Kitime (picha ndogo) ameingiza utani kwenye jambo hilo kwa kumlaumu kulifanya kuwa la siri kama kweli lipo.
Kupitia blog yake mzee Kitime aliandika hivi: “Mimi na Watanzania
wenzangu tumepata mshtuko baada ya kusoma habari hii. Mpaka sasa
tunajiuliza ‘why Jokate Why?’
“Wewe unaelewa taratibu kuwa mtu anapotaka kuchumbiwa huwa haifanywi siri.
“Jambo la kwanza unaenda kwa afisa utamaduni kuomba kibali ambacho
unatakiwa kukipitisha vituo vya polisi vya jirani kisha kibali hicho
kupigwa mhuri na katibu mtendaji wa kata unayotegemewa kuchumbiwa na
hatimaye kupitia kwangu Afisa Vibali vya Kuchumbiwa, ambapo nitaita
Press Conference kutangaza uchumba. Umevunja sheria namba 6 ya 1956 ya
Uchumbalization Act...
No comments:
Post a Comment