Wacheza filamu wenye majina makubwa Bongo, Wema Sepetu na Aunt Ezekiel wadaiwa kuwa na bifu kubwa kwa sasa. inasemekana
bifu hilo lilianza kwenye mkesha wa mwaka mpya baada ya aunt kutofika
kwenye sherehe ya kukaribisha mwaka mpya iliyoandaliwa nyumbani kwa Wema
licha ya kukubali mwaliko.
Ilipotimu saa 6:01 usiku bila ya Aunt kuonekana, Wema alimtumia ujumbe mzito kupitia BBM na Aunt akaanza kuomba radhi na ujumbe
wa Wema ulisomeka hivi: “Hata sina hamu na wewe ila Happy New Year,
sihitaji samahani yako sijui niku-delete?”akimaanisha amfute BBM.
Inasemekana
Wema alikasirika na kuhisi kwamba Aunt aliungana na baadhi ya wasanii
wengine wa Bongo Movie ambao hakuwaalika kwenye shughuli yake kutokana
na kupishana nao
Kiswahili siku za nyuma.
Asubuhi
ya mwaka mpya, Aunt aliandika kwenye mtandao wa BBM maneno ya kuomba
radhi kwa wema; “ Chondechonde my luv, nimekosea mamy naomba unisamehe,
naomba msamaha mbele ya hadhara.”. juhudi za kuomba radhi azikuzaa matunda kwan Wema hakujibu kitu zaidi ya kumpotezea rafiki yake huyo
Source: Zeddylicious
No comments:
Post a Comment